Michezo
Hiki hapa kikosi cha Yanga SC, Ajib, Chirwa, Tshishimbi ndani
Klabu ya soka ya Yanga imekiweka wazi kikosi chake kitakachoshuka dimbani hii leo katika mchezo wa ligi kuu kuvaana na wana lamba lamba Azam FC uwanja wa Azam Complex.
Kuelekea katika mchezo huo msemaji wa klabu ya Yanga, Dismas Ten hapo jana amesema wachezaji saba wa kikosi hicho watao ukosa mmchezo huo ambao ni Yohana Mkomola,Pius Buswita,Thaban Kamusoko,Amissi Tambwe,Abdallah Shaibu,Donald Ngoma na Patongonyani wote ni wagonjwa pamoja na kuumwa Pius Buswita anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano.