Burudani

Jay Z, Beyonce, Nicki Minaj, Usher na mastaa wengine kutumbuiza kwenye show ya charity ya Tidal

Baada ya mtandao wa Tidal kufikisha zaidi ya watumiaji milioni moja, Jay Z aliahidi kusheherekea na sasa ametangaza shangwe hizo zitakuwa lini na wapi.

tidal

Jay ametangaza show za charity za TIDAL X: 1020 ambapo kwa mara ya kwanza itafanyika Oct. 20 kwenye uwanja/ukumbi wa Barclays Center, Brooklyn.

Pamoja na Jay Z mwenyewe, mastaa wengine watakaotumbuiza ni pamoja na Beyoncé, Prince, Nicki Minaj, Usher, Lil Wayne, na T.I. Wengine ni Nick Jonas, Damian Marley, Fabolous, Alessia Cara, Bas na Justine Skye.

Tiketi za show hiyo zitauzwa kuanzia $74 na $244. Show hiyo itaonekana live kupitia TIDAL.com na HTC.com.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents