JB atoa ushauri kwa waigizaji wa kike, asema wengi hawako ‘serious’
Muigizaji, mtayarishaji na muongozaji wa filamu, Jacob Stephen aka JB, amesema waigizaji wengi wa filamu wa kike hawako serious.
JB akiwa location kushoot video yake ijayo, Mzee Swagga
JB ambaye kupitia kampuni yake, Jerusalem Films, aliongoza filamu aliyoigiza Shamsa Ford, Chausiku inayotajwa miongoni mwa filamu bora za mwaka huu, amesema waigizaji wa kike wanashindwa kutumia umaarufu wao kufanya filamu bora.
“Majina yao ni makubwa sana lakini useriousness kwenye filamu ni mdogo sana,” JB ameiambia Bongo5.
“Kwa majina yao makubwa, tungeshirikiana nao kwa ukubwa ule na wakawa serious, film industry ingekuwa mbali sana kuliko hapa tulipo. Mimi nawaasa tu, wana kipaji kikubwa, wawe serious na waweke akili yao kwenye kazi hii na watafanikiwa.”
JB aliongeza kuwa wasanii hao wengi wao wanapendwa hivyo kazi yao ni rahisi zaidi kama watajituma na kupenda kazi yao iliyowapa majina.