Burudani
Je, toka afanye ngoma na Alikiba Papaa Masai yupo wapi??
Huyu ni msanii aliyeanza Muziki miaka kadhaa nyuma na aliwahi kufanya kazi na Alikiba kupitia Ngoma yake ya Ng’aring’ari miaka kadhaa iliyopita.
Mbali na Alikiba pia Papaa Masai amewahi kufanya kazi na kundi la Yamoto Band kwenye ngoma ya (Mtoto wa Kariakoo).
Kuna muda Papaa Masai alikaa kimya lakini ghafla aliibuka na ngoma kadhaa zinazofanya kazi vizuri ambazo kaimba kwa lugha ya kabila lake Kimasai.
Huyu ni Msanii anayetoka Umasaini huko nchini Kenya na anafanya vizuri kupitia ngoma zake hizo za kimasai.
Papaa Masai ana ngoma zake mbili hapo NANARE na NYOOLO IYOOK ambazo kaimba kwa Kimasai.
Unamshauri nini?? Aendelee na kuimba Kimasai au arudi kwenye muziki wake wa Zamani??
Imeandaliwa ma El_mando_tz.
Imeandikwa na Mbanga B.