Michezo
#KariakooDerby: Simba SC na Yanga zatoshana nguvu Uwanja wa Taifa
Klabu ya Simba imetoshana nguvu na klabu ya Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Soka Tanzania uliochezwa kunako dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.
Mchezo huo ulianza kwa kasi ambapo Simba ndio walikuwa wanamiliki mpira karibia vipindi vyote kwa asilimia 80 na kutinga golini mara nyingi kuliko Yanga.