Kifaa kinachodhaniwa kuwa kinalipuka chabainika nyumbani kwa Barack Obama na Hillary Clinton
Kifaa kinachosadikiwa kuwa ni mlipuko kimebainika katika nyumba kwa Hillary Clinton na Barack Obama hii leo, maafisa wa sheria wameiviambia vyombo vya habari nchini Marekani.
Aina kama hiyo ya kifurushi kinachoshukiwa kimetaarifiwa kutumwa pia katika jengo la Time Warner jijini New York.
Ni siku mbili baada ya bomu kurushwa katika nyumba ya mfadhili na mshauri wa mambo ya fedha George Soros huko mjini New York.
Clinton ambaye ni rais wa zamani wa Marekani na mke wake Bi.Clinton ambaye aliwania urais mwaka 2016. Taarifa zilizoripotiwa na New York Times zimesema kwamba kituo hicho kilibainika kuwa kinalipuka baada ya fundi kukifanyia uchunguzi.
Kifaa hicho kiliachwa kilomita 65 kaskazini mwa mji wa New York.
Haijawekwa wazi kuwa kifaa hicho kinachotiliwa shaka kilionekana wapi.
Kwa mujibu wa shirikisho la habari la BBC, msemaji wa Obama amekana kuwepo kwa tukio hilo na kuwataka waandishi kushirikiana na idara ya huduma ya maelezo ya siri.
Maafisa wakuu wa White House wameiambia NBC kwamba rais Donald Trump tayari ameshapata taarifa kuhusu jambo hilo.
We condemn the attempted attacks against fmr Pres Obama, the Clintons, @CNN & others. These cowardly actions are despicable & have no place in this Country. Grateful for swift response of @SecretService, @FBI & local law enforcement. Those responsible will be brought to justice.
— Vice President Mike Pence Archived (@VP45) October 24, 2018
Msemaji wa Ikulu Sarah Sanders amelaani jaribio hilo la mashambulio ya vurugu dhidi ya watu mashuhuri.
“Matukio ya kigaidi hayakubaliki popote na mtu yeyote ambaye atakamatwa kuhusika atachukuliwa sheria
Uchunguzi bado unaendelea ili hatua sahihi ziweze kuchukuliwa” Msemaji wa Whitehouse Sarah Sanders .
The Time Warner Center (CNN’s NYC bureau) has been evacuated. Jeff Zucker sent the following note to staff. No additional comment or details at this time. Watch CNN for developments. pic.twitter.com/m0Pd2JIwOA
— CNN Communications (@CNNPR) October 24, 2018