Michezo
Kipa wa Man City aliyechanika uso apangwa dhidi ya Feyenoord Uefa
Mlinda lango wa klabu ya Manchester City, Ederson Santana de Moraes amehujumuishwa katika kikosi kitakacho cheza mchezo wa ufunguzi wa michuano ya klabu bingwa barani Ulaya dhidi ya Feyenoord siku ya Jumatano.
Ederson mwenye umri wa maiaka 24,alipata majeraha katika sehemu ya paji la uso hivi karibu baada ya mchezaji wa Liverpool, Sadio Mane kumpiga teke la uso walipocheza siku ya Jumamosi huku City kuchomoza na ushindi wa mabao 5-0.
Mapema hii leo kipa huyo raia wa Brazili ameonekana katika mazoezi na timu yake ya Man City huku akiwa amevalia kilinda kichwa katika maeneo aliyojeruhiwa.