Lawrence Okolie aahidi kumzimisha Chamberlain usiku wa Jumamosi
Kuelekea pambano la masumbwi hapo kesho siku ya Jumamosi, bondia Lawrence Okolie amemuonya mpinzani wake Isaac Chamberlain kuwa atarajie kupata maumivu makali kunako ulingo.
Lawrence Okolie na Isaac Chamberlain wanatarajiwa kuingia ulingoni usiku wa Jumamosi hii katika uwanja wa The O2 nchini Uingereza.
Kwa upande wake Chamberlain ameahidi ushindi kwa gharama yoyote dhidi ya bondia huyo hasiye pigika huku Okolie akisisitiza kumchakaza wikiendi hii.
Pambano hilo linalo simamiwa na promota maarufu nchini Uingereza, Eddie Hearn’s Matchroom Boxing kwa kushirikiana na Anthony Joshua’s AJ BXNG unaweza kujipatia bei ya tiketi yako HAPA.
These 2 fighters have come a LONG way! Respect to them for putting everything on the line… Expect fireworks come Saturday night 💥💥 #TBT #StayHungry pic.twitter.com/8iMWh0FPej
— Anthony Joshua (@anthonyjoshua) February 1, 2018