Majina 40 ya vijana wanaowania tuzo ya UEFA Golden Boy 2016
Shirikisho la soka barani Ulaya,UEFA, limetoa orodha ya wachezaji 40 watakaowanaia tuzo ya mchezaji bora wa mwaka kwa wachezaji walio na umri wa chini ya miaka 21 maarufu kama UEFA Golden Boy Award.
Marcus Rashford
Kelechi Iheanacho
Ligi kuu za England na Ujerumani zimeongoza kwa kutoa wachezaji wengi katika kinyang’anyiro hicho chenye hadhi kubwa zaidi Ulaya kwa wachezaji vijana.
Baadhi ya wachezaji wa ligi kuu ya England waliobahatika kupenya kwenye kinyang’anyiro hicho ni pamoja na Marcus Rashford,Dele Alli na Alex Iwobi.Wengine ni Ruben Loftus-Cheek,Marko Grujic Kelechi Iheanacho na Leroy Sane.Ujerumani ni Julian Brandt Andreas Christensen Kingsley Coman na Mahmoud Dahoud.
Christensen Kingsley Coman
Wachezaji wengine ambao waliwahi kushinda hiyo tuzo huko nyuma ni pamoja na Lionel Messi,Sergio Aguero,Raheem Sterling na Paul Pogba.
Orodha Kamili ya wachezaji 40 hii hapa