Michezo
Matokeo ya mechi za Europa League zilizochezwa Alhamisi October 20
Michuano ya EUROPA League iliendelea usiku wa October 20 2016, jumla ya michezo 24 ambayo ilichezwa katika viwanja tofauti tofauti barani Ulaya.
Mtanzania Mbwana Samata
Timu ya Genk ambayo anaichezea Mtanzania Mbwana Samata iliibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Atletico Bilbao na kukusanya pointi tatu wakiutumia vyema uwanja wao wa nyumbani Cristal Arena, Samatta aliingia dakika ya 56 kipindi cha kuchukua nafasi ya Thomas Buffel.
Manchester United nao waliibuka na ushindi mnono wa 4-1 dhidi ya klabu ya Fenerbahce katika kundi A.
Matokeo ya mechi zote za Europa League zilizochezwa Alhamisi October 20