Mduara wa Diamond na Khadija Kopa waingia kwenye Top 10 ya Radio ya Lagos, Nigeria
Diamond Platnumz kupitia wimbo wake ‘Nasema Nawe’ ametuthibitishia kuwa msanii wa Tanzania anaweza kufanya wimbo wenye mahadhi ya kwetu na bado ukapokelewa kwa ukubwa ule ule na mataifa mengine. Wimbo wake aliomshirikisha malkia wa Taarab, Khadija Kopa umeingia kwenye Top 10 ya Radio ya Nigeria.
‘Nasema Nawe’ imekamata namba saba kwenye African Top 10 ya The Beat 99.9 FM ya Lagos, Nigeria.
#MorningRush #AfricanTop10 #DemocracyDay with @MariaOkan, @OfficialOlisa No.7: "Nasema Nawe Ft. Khadija Kofa " – @diamondplatnumz
— THE BEAT 99.9FM (@THEBEAT999FM) May 29, 2015
Mtanzania mwingine ambaye yuko kwenye chati hiyo ni Vanessa Mdee ambaye wimbo aliomshirikisha rapper K.O wa Afrika Kusini umeendelea kushika namba moja.
#MorningRush #AfricanTop10 #DemocracyDay with @MariaOkan, @OfficialOlisa No.1: "Nobody But Me Ft. @MrCashtime " – @VanessaMdee (RSA/TAN)
— THE BEAT 99.9FM (@THEBEAT999FM) May 29, 2015
Hii inatoa somo kwa wasanii wetu kuwa sio lazima wasanii kufanya nyimbo zenye mahadhi ya Kinigeria au kutumia lugha ya kiingereza ili kuweza kufanya vizuri kwenye soko la kimataifa.