Burudani

Msanii huyu pia adai kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya

Msanii aliyewahi kuhit na wimbo ‘Kazi ya Duka’, Dogo Mfaume amedai kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya.

DSCN7359

Anadai kuwa ujana na makundi vilimfanya ajiingize kwenye utumiaji wa madawa hayo. Ameiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM Alhamis hii kuwa wengine hutumia madawa ya kulevya kuwaongezea nguvu za kufanya mapenzi na kujikuta wakinaswa kabisa.

“Kusema ukweli mimi nimetumia kwa miaka miwili na nusu,” amesema.

Anadai hiyo ni sababu kubwa iliyomfanya apotee kabisa kwenye muziki kwakuwa kabla hajaanza alikuwa na uwezo mzuri wa kutunga nyimbo lakini ulipotea.

Msikilize hapo chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents