Burudani
Msanii huyu pia adai kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya
Msanii aliyewahi kuhit na wimbo ‘Kazi ya Duka’, Dogo Mfaume amedai kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya.
Anadai kuwa ujana na makundi vilimfanya ajiingize kwenye utumiaji wa madawa hayo. Ameiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM Alhamis hii kuwa wengine hutumia madawa ya kulevya kuwaongezea nguvu za kufanya mapenzi na kujikuta wakinaswa kabisa.
“Kusema ukweli mimi nimetumia kwa miaka miwili na nusu,” amesema.
Anadai hiyo ni sababu kubwa iliyomfanya apotee kabisa kwenye muziki kwakuwa kabla hajaanza alikuwa na uwezo mzuri wa kutunga nyimbo lakini ulipotea.
Msikilize hapo chini.