Mtangazaji maarufu wa SuperSport Tv, Robert Marawa afukuzwa kazi juu kwa juu, Mashabiki wake wamuita shujaa kwa kupinga unyanyasaji wa kijinsia
Mtangazaji maarufu wa michezo katika kituo cha SuperSport TVnchini Afrika Kusini, Robert Marawa amefukuzwa kazi na kituo hicho muda mchache kabla ya kwenda hewani siku ya Jana kwenye kipindi cha Thursday Night Live.
Robert Marawa amethibitisha taarifa hizo kupitia ukarasa wake wa Twitter kwa kueleza kuwa alitumiwa ujumbe mfupi na Mabosi wake kuwa asifike ofisini kwenye kipindi cha TNL kwani mkataba wake umeisha.
Kufuatia tukio hilo, Supersport wametoa tangazo kuwa wanatarajia kufanya mabadiliko ya watangazaji wa ndani kwa kuangalia upya marekebisho ya baadhi ya mikataba ikiwemo wa Robert Marawa.
SuperSport is in the process of an exciting refresh of its local presenter line-up, which will be unveiled as part of our new football season campaign. This restructure includes us not pursuing our contractual relationship with Robert Marawa. (1/2)
— SuperSport 🏆 (@SuperSportTV) May 17, 2019
Duru za habari nchini Afrika Kusini, zinaeleza kuwa Mtangazaji huyo kupitia ukurasa wake wa Twitter siku tatu zilizopita aliandika ujumbe ulioashiria kuwa kuna baadhi ya makampuni makubwa yanawalipa watu wanaofanya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.
Robert Marawa ni moja ya watangazaji wa michezo wanaovutia zaidi kuwasikiliza, hususani kwa wale watu wanaofuatilia michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya na Kombe la Mataifa huru Afrika.
Ameshawahi pia kutangaza kipindi cha Sports Zone cha Shirika la Habari Afrika Kusini (SABC) na baadae alifukuzwa kisha akajiunga na SuperSport.
Hatua hiyo ya kufukuzwa kwake imepokelewa na baadhi ya mashabiki kama’ ushujaa’ kwani ameongea vitu ambavyo anaona haviko sawa.
#RobertMarawa once took a bullet for his producer who was suspended from the SABC and he got fired. Now he took a bullet for the interns who are sexually abused by the "Top Dogs" and he got fired again. But they don't know that You Can't Keep The Good Man Down, he'll rise again
— Sbuda (@Sbuda_H) May 17, 2019
https://twitter.com/BongiBMbele/status/1129125664953634822
Robert Marawa being fired for fighting against sexual harassment at work place ,he doesn't only talk the talk ,he walk the talk ,he is a principled man & would rather speak than letting injustice and abuse of women take place around him ,I stan ,we need more Robert Marawas in SA
— Major General (@EliasChinemore) May 16, 2019