Baadhi ya wasanii wa Kanda ya Ziwa wameungana na kufanya wimbo wa pamoja kwa ajili ya kupiga mauaji ya albino kwa mikoa ya kanda hiyo, Tanzania na dunia nzima. Wasanii walioshiriki katika wimbo huo wa “Tuwaonee Huruma” ni pamoja na Kala Jeremiah, Baraka Da Prince, Gabriel Ng’osha ‘Mlapa Ng’osha’, Leah Musa ‘Shasta’ Fatuma ‘Bi Mwenda’, Kulwa Kikumba ‘Dude’ , PNC, Bond, Noorah, Edger, Nicole Sarakikya ‘Miss Shinyanga-2004.
Wimbo huo umefanywa katika studio za plexity rekodi chini ya prodyuza Zest mkali.