Mitindo
Ommy Dimpoz ashinda tuzo ya Swahili fashion
Katika wiki ya Swahili fashion ambayo ilifanyika kuanzia siku ya jumamosi na kumalizika usiku wa kuamkia leo katika hotel ya Serena staa wa Bongo Fleva Omary Nyembo alimaarufu Ommy Dimpoz amefanikiwa kushinda tuzo ya mwanamitando bora wa kiume.
Tuzo hiyo ya Men Stylish Personality ya mwaka 2021 ilikuwa inagombaniwa na mastaa kadhaa wakiwemo muigizaji Rammy Galis, Rich Mitindo, Jimmy Chansa, Quick Rocka, Maxi Rioba na Jamal April.