Burudani
P Funk amchana Marioo juu ya Mahusiano na Paula (Video)
P Funk ametoa nasaha kwa vijana wake Marioo na Paula kuwataka wakaishi kwa Upendo na wadumu kwenye ndoa.
P Funk ametoa kauli hiyo jana April 17, 2024 kwenye Baby Shower ya binti yake huyo ambaye anatarajia kujifungua hivi karibuni.
Akimuelekeza Marioo P Funk alimwambia awe Baba Bora.
“Omari (Marioo) ninakuombea uwe Baba Bora na uwe mume bora muweze kudumu kwenye ndoa yenu kama ilivyo yangu ina miaka 14 hivi sasa” alisema P Funk.
Imeandikwa na Mbanga B.