Penzi la Soulja Boy na Blac Chyna laacha historia Marekani, mrembo afunguka ‘hana lengo, alitaka kuchungulia nilivyoumbika’
Ukitaja mahusiano ya wasanii na watu maarufu nchini Marekani yaliyodumu kwa muda mfupi, basi ni penzi jipya kati ya rapper Soulja Boy na mwanamitindo Blac Chyna huenda likaingia kwenye rekodi, baada ya wawili hao kumwagana ndani ya wiki mbili.
Wawili hao wiki iliyopita kwenye siku ya wapendanao walikuwa sambamba na waliudhihirishia umma kuwa wapo kwenye mahusiano.
Sasa kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, umeeleza kuwa wawili hao tayari wamemwagana na kila mmoja amechukua hamsini zake.
Chanzo kimeelezwa kuwa Soulja Boy alimtongoza Blac Chyna kwa lengo la kumuumiza rapper mwenzie, Tyga ambaye alishawahi kuwa na mahusiano na mrembo huyo.
Tyga kwa sasa na Soulja Boy ni Chui na Paka. Na imeelezwa kuwa Soulja Boy alimlipa Blac Chyna dola $20,000 sawa na Tsh Milioni 47 ili kutoka naye siku ya Valentine.
Wakati hayo yakijiri, mrembo Blac Chyna naye ali-tweet na baadae kufuta Tweet hiyo ambapo aliandika ‘he just wanted to see what the p***y felt like‘ akimaanisha kuwa Souja Boy alitaka tu kumchezea kwa kumuangalia maumbo yake hakuwa na lengo nae.
Blac Chyna katika maisha yake ya umaarufu, alishawahi kuwa kwenye mahusiano na rapa Tyga, Kid Buu na Rob Kardashian .
Tayari Soulja Boy, amemtangaza mwanamke mwingine ambaye amekiri kuwa huyo ndiye atakayedumu naye .