Picha: Diamond aondoka nchini kurejea London kwenye show nyingine leo (May 17)
Baada ya kuzikonga nyoyo za mashabiki wa Dar es salaam usiku wa kuamkia leo pale Club Billicanaz, Diamond Platnumz ameondoka nchini alfajiri ya leo kurejea tena London, Uingereza anakotarajiwa kufanya show nyingine usiku wa leo (May 17) akiwa na Ommy Dimpoz aliyemuacha huko.
LONDON!!! LONDON!!! LONDON!!! I thout i told ya … see you in a bit -Diamond
Platnumz aliingia nchini jana Ijumaa (May 16) akitokea Uingereza kama alivyoahidi na kuhudhuria show ya MTV Africa Road to MAMA iliyofanyika Club Billicanas usiku wa kuamkia leo. Akiwa London Platnumz aliahidi kurejea nchini kwaajili ya tukio hilo muhimu, akiwa kama nominee wa tuzo za MTV Africa (MAMA).
Platnumz ameshare picha akiwa uwanja wa ndege alipokuwa akijiandaa kucheck in mida ya saa 9 alfajiri.
president @diamondplatnumz off to London for another show tonight-wcb_wasafi