Burudani

Picha: Godwin ‘Double G’ Gondwe ahamia Clouds FM/TV?

Vijana wa mjengoni aka Clouds Media Group wiki hii walikuwa ‘chimboni’ jijini Arusha ambako walienda kutengeneza mikakati ya namna ya kuingia kwa nguvu kwenye jukwaa jipya la utengenezaji wa ‘content’ kwenye mfumo wa dijitali zaidi.

cmg
Watangazaji wa Clouds FM wakiwa Arusha

Tulishamsikia Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Joseph Kusaga akielezea kuingia kwenye mfumo uitwao ‘Over the Top’ OTT so nahisi ziara hiyo ya Arusha ilikuwa ni kwaajili ya kujipanga zaidi.

Vijana hao wanarejea Dar es Salaam kuendelea na majukumu yao ya kila siku but guess what (kwa sauti ya Dee Andy).. inaonekana mtangazaji mkongwe aliyewaHi kutangaza Radio One, RFA na sasa akiwa msomaji wa habari wa ITV, Godwin Godwin aliungana na vijana wa mjengoni jijini Arusha.

1978895_832750000074664_829159781_n
Kutoka Kushoto: Millard Ayo, Mbwiga wa mbaaaali, Perfect Crispin, Gerald Hando na Godwin Gondwe

Godwin ameonekana na watangazaji hao wakiwa kwenye uwanja ndege wa Arusha kurejea Dar.

1960114_832749270074737_247259783_n
Kutoka Kushoto: Mbwiga, Millard Ayo, Perfect Crispin, Gerald Hando na Godwin Gondwe (huyo mwingine sijui nani!!)

Picha hiyo inazalisha maswali mengi iwapo Double G ameungana na Clouds Media Group ama ni abiria tu kwenye ndege hiyo na aliamua kupiga picha nao…

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents