Habari
Picha: Wananchi walivyofurika kwenye uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa
Maelfu ya wananchi Jumatano hii wamejitokea kwenye uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt John Magufuli alikuwa mgeni.
Muitikio huo mkubwa wa wananchi katika uwekwaji jiwe la msingi kwenye eneo Pugu ni ishara ya kuwa walikuwa wanahitaji kusikia jambo kutoka kwa Rais Magufuli pamoja na kushuhudia ujenzi huo wa reli ya kisasa.
Watu walikuwa wamefurika kila pande kiasi kwamba wengine walipanda juu ya vilima ili mradi waweze kushuhudia.
Hizi ni baadhi ya picha za wananchi walivyofurika:
Na Emmy Mwaipopo