Habari

Picha za utupu za mgombea urais Rwanda zavuja mtandaoni

Baada ya siku chache za Diane Shima Rwigara kutoka Rwanda kutangaza kugombea urais nchini humo, hatimaye amekutwa na skendo ya kuvujisha picha zake za utupu mtandaoni.

Image result for Diane Rwigara
Mrembo Diane Rwigara pichani aliyeshika Mkoba,Akiwasili ukumbini alikoenda kutangaza nia ya Kugombea urais.

Diane 35, ambae ni msomi wa Uchumi na mtoto wa aliyekuwa tajiri maarufu nchini Rwanda Asinapol Rwigara, picha zake za utupu zilianza kusambaa mapema jana nchini Rwanda hususani kwenye mitandao ya kijamii kama WhatsApp na Facebook na baadae kutapakaa duniani kote.

Kwa mujibu wa mtandao wa Habari Pevu umeeleza kuwa picha hizo zilitumwa awali kwa njia ya e-mail na mtu aliyejiita ni Muandishi wa habari aliyejulikana kwa jina la Twahirwa Emmy huku akishinikiza kuwa mrembo huyo hafai kuchaguliwa kuwa Rais kwa vitendo vyake  vichafu vya kupiga picha za utupu.

                                          Mrembo Diane Rwigara akiwa mtupu .
                                          Diane Rwigara akiwa kwenye pozi

Hata hivyo Jitihada za kumpata mrembo huyo kuzungumzia picha hizo zilizovuja ziligonga mwamba baada ya waandishi wa habari nchini Rwanda kumsaka bila mafanikio.

Uchaguzi mkuu wa Rais nchini Rwanda unatarajiwa kufanyika mwaka huu mwezi wa Augosti, na mpaka sasa kuna wagombea watatu tuu ambao ni Mpayimana Philippe ambae ni mgombea binafsi na Franck Habineza kutoka chama cha Green pamoja na Diane Rwagira wote wakitarajiwa kuleta upinzani mzito kwa Rais Paul Kagame .

Mtandao wako wa Bongo5 utakuletea kila tukio litakalotokea nchini Rwanda kuelekea uchaguzi mkuu nchini humo.

By Godfrey Mgallah

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents