Burudani
Priyanka Chopra akimbizwa hospitali baada ya kuumia akiigiza kwenye Quantico
Staa wa Quantico, Priyanka Chopra amelazimika kukimbizwa hospitali baada ya kuumia wakati akiigiza kwenye tamthilia hiyo.
Vyanzo vimeuambia mtandao wa TMZ kuwa Priyanka alipelekwa hospitali Alhamis usiku baada ya kuteleza na kuangukia kichwa. Priyanka alifanyiwa uchunguzi, alitibiwa na kuruhusiwa kuondoka baadaye.
Msemaji wake alidai kuwa Priyanka anapumzika kwa sasa na ataendelea na kazi wikiendi hii.