Burudani
Rapper huyu wa Young Money afungwa jela mwaka mmoja
Rapper Lil Twist atachezea ndoo za jela.
Jumatano hii, rapper huyo wa Young Money alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kudaiwa kuvunja nyumba ya muigizaji wa zamani wa Nickelodeon, Chris Massey na kuiba Rolex yake na kumpiga mwaka 2014.
Akiwa na umri mdogo, rapper huyo alijiunga na Young Money na kuwa na urafiki na Justin Bieber. Maisha yake yalitawaliwa na kashfa nyingi. Mwaka 2013, rapper huyo alikamatwa akiendesha akiwa amelewa gari la Bieber.
Twist ataingia jela Feb. 3 na anaweza kuachiwa huru mwezi August iwapo ataonesha tabia nzuri.