Technology
Samsung yazindua ‘Galaxy Gear’ smartwatch unayoweza kupiga simu, kutweet, kuinstagram nk
Sasa unaweza ukatweet au kujibu email kupitia saa yako ya mkononi. Hata hivyo, ili kufanya hivyo itakubidi uwe na Galaxy Gear, smartwatch Samsung.
Samsung wamezitambulisha saa hizo ambazo unaweza kupiga simu ama kutumia apps mbalimbali, kama tu ilivyo kwenye simu.
Saa hizo zilikuwa zikisubiriwa kwa hamu kubwa hasa kwakuwa Samsung sasa ndio watengenezaji wa simu zinazouzwa zaidi duniani wakiwazidi Microsoft, Apple na Google kuzindua kifaa kama hicho.