Michezo

TP Mazembe ya Ifunga 1-0 Zamalek na Kuongoza Kundi A

Club ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliishinda Zamalek ya Misri kwa goli 1-0 kwenye mechi za makundi ya Ligi Kuu ya Mabingwa Afrika siku ya June 8 Jumapili

10390573_759354270753535_4624292855848683199_n

Mchezaji kutoka Zambia Rainford Kallaba alifunga goli pekee lililoipa ushindi TP Mazembe. Kwa matokeo hayo ya Lubumbashi yanamaanisha kwamba Mazembe wanaongoza kundi A kwa alama sita.

Wenzao wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, AS Vita Club wako nafasi ya pili, wakipitwa kwa alama mbili.

AS Vita walitoka sare ya 1-1 dhidi ya timu ya Sudan Al Hilal siku ya Ijumaa.

Kwa upande wa kundi B, Entente Setif ya Algeria walibanwa mbavu kwa sare 1-1 nyumbani kwao na Al Ahli Benghazi ya nchini Libya.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents