Habari

Tundu Lissu kufanyiwa upasuaji mwingine leo

Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwingine siku yao.

Tundu Lissu yupo katika matibabu nchini Ubelgiji mara baada ya kushumbaliwa kwa kupingwa risasi na watu wasiojulikana September mwaka jana mjini Dodoma.

“Kama nilivyowataarifu siku za nyuma, mguu wa kulia bado una shida kutokana na risasi nyingi nilizopigwa na ‘watu wasiojulikana, operesheni ya leo ni sehemu ya tiba ya mguu huo. Napenda wote mfahamu kwamba niko kwenye mikono salama ya kitabibu. Mungu wetu amekuwa mwema sana kwangu tangu tarehe 7 September ya mwaka jana,” amesema Tundu Lissu.

Kabla ya kupelekwa Ubelgiji kwa ajili ya matibu zaidi, Lissu alikuwa akipokea matibabu Nairobi nchini Kenya ambapo December 26 aliweza kusimama kwa mara ya kwanza tangu aliposhambuliwa. January 07, 2018 ndipo aliwasili Ubelgiji.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents