Burudani
Umeiona video ya wimbo mpya wa Kiswahili wa Bobi Wine? Icheck hapa
Msanii maarufu wa Uganda, Bobi Wine ameachia video ya wimbo wake mpya alioimba kwa Kiswahili 100% uitwao, Paradiso.
Wimbo huo unazungumzia umuhimu wa wazazi, na ameutoa mahsusi kwa wazazi wake ambao walishafariki.
Anasema kuwa marehemu baba yake, Sentamu ndiye aliyekuwa akimwambia mara kwa mara kuimba kwa Kiswahili lakini msanii huyo anayejiita Ghetto President hakuweza kutilia maanani kwakuwa aliona kuna wasanii wengine kama Jose Chameleone wanaoifahamu lugha hiyo vyema na hivyo hakutaka kujiabisha.
Itazame video hiyo hapo juu, utaipenda.