Rais Vlamidir Putin wa Uurusi amesema hapo jana kuwa kunauwezekano wa kuongeza maradufu thamani ya biashara kati ya Urusi na Afrika katika kipindi cha miaka minne au mitano inayokuja.
Putin ametoa matamshi hayo wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa kilele wa siku mbili kati ya Urusi na Afrika unaofanyika kwenye mji wa mapumziko wa Sochi.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Deutsche Welle, Biashara kati ya pande hizo mbili tayari imeongezeka maradufu katika kipindi cha maika mitano na kufikia thamani ya dola bilioni 20 za Marekani, kiwango ambacho Putin amekitaja kuwa kidogo.
Moscow ilikuwa na ushawishi mkubwa barani Afrika wakati wa enzi ya kisovieti kwa kuunga mkono juhudi za kutafuta uhuru pamoja na kutoa mafunzo kwa viongozi wa kiafrika.