Michezo
Video: Leon wa Everton apewa heshima hii
Leon Osman amepata zawadi kutoka Hifadhi ya Taifa ya Manyara pamoja Bendera ya Tanzania na kumpa heshima ya kuwa balozi wa Utalii Tanzania.
Leon Osman ameendelea kutembelea vivutio mbali mbali hapa nchini kabla ya mchezo wa Everton FC dhidi ya Gor Mahia wa kuhitimisha michuano ya SportPesa Super Cup utakaochezwa Julai 13 katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Viingilio vya mchezo huo ni Sh 8000/= kwa VIP C na Sh 3000/= kwa viti vya mzunguko na mchezo unatarajiwa kuanza majira ya saa 11 jioni.
By Hamza fumo