Habari
Wanafunzi wafunga barabara
Baadhi ya wazazi na wanafunzi mchana huu wamefunga barabara kwa kuweka magogo maeneo ya mtongani kunduchi. Haya yametokea baada ya wanafunzi watatu kugongwa na gari kwenye barabara hiyo na kusababisha foleni kubwa na magari kutopita.Baadhi ya magari yaendayo bahari beach kupitia njia ya tegeta yamejikuta yakikwama njiani kutokana na tukio hilo.
Wazazi,wanafunzi na wakereketwa pamoja na kuweka magogo walitaka kuongezea matuta zaidi katika eneo hilo. Jeshi la polisi lilifika mapema zaidi kutuliza fujo hizo kubwa zilizotokea kwa kurusha mabomu ya machozi.
Mpaka Bongo5 inakwenda mitambo haikuweza kugundua hali ya wanafunzi hao iko vipi na gari liliweza kupatikana. Tutazidi kufuatilia tukio hili na kukuhabarisha zaidi.