Habari
WHO: Nigeria haina tena Ebola
Shirika la afya duniani, WHO, leo limetangaza kuwa Nigeria haina tena ugonjwa wa Ebola.
Hatua hiyo imedaiwa kama ushindi na shirika hilo.
Nigeria iliripoti kesi 20 za Ebola pamoja na vifo nane tangu ugonjwa huo ulipuke. Miongoni mwa watu waliofariki ni pamoja na abiria wa ndege aliyeupeleka ugonjwa huo nchini Nigeria na kufariki baadaye kidogo.
Ugonjwa huo bado unaendelea kusambaa kwa kasi katika nchi za Liberia, Sierra Leone na Guinea na umeshaua zaidi ya watu 4,500.