Michezo
Rhino Rangeres yaitunishia misuli Yanga SC
Timu ya soka ya Yanga imetoka sare ya bila kufungana dhidi ya Rhino Rangeres katika mchezo wa kirafiki uliyochezwa hii leo siku ya Jumatano kwenye Uwanjanwa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.
Yanga SC imetumia mchezo huo kama sehemu ya maandalizi yao ya ligi kuu dhidi ya Stand United wikiendi hii, imetumia zaidi wachezaji wake wa kikosi cha pili.
Yanga SC inakabiliwa na kibarua kizito Octoba 28 mwaka huu pale itakapoingia Uwanjani kuvaana na mabingwa wa kombe la FA klabu ya Simba katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.