Zinedine Zidane kurithi mikoba ya Mourinho Manchester United
Aliyekuwa meneja wa Real Madrid, Zinedine Zidane ameoneshania ya kuhitaji kuifundisha klabu ya Manchester United na kurithi mikoba ya Jose Mourinho msimu ujao wa ligi.
Kwa mujibu wa gazeti la L’Equipe kutoka nchini Ufaransa Daily Mil, METRO na Mirror vimesema kuwa Zidane anajipanga kutua ligi ya Uingereza hasa ndani ya klabu ya Manchester United.
Zidane ambaye ni raia wa Ufaransa aliiyacha klabu yake ya Madrid baada ya kuipatia jumla ya mataji matatu mfululizo ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.
Mfaransa huyo aliwahi pia kuhusishwa na kuhitaji kuinoa timu yake ya taifa lakini meneja Didier Deschamps aliamua kuendelea na majukumu yake mara baada ya kutwaa ubingwa wa dunia nchini Urusi.
Mourinho ameingia kwenye mgogoro na makamu mwenyekiti wa Old Trafford, Ed Wood kwenye kipindi cha maandalizi ya kuanza msimu mpya ligi kufuatia kulalamikia kukosa kusajili wachezaji wliyowahitaji.
Historia yake ya kutomaliza misimu mitatu ndani ya klabu moja imekuwa nichangamoto kubwa kwa Mreno huyo, hata hivyo amefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabo 2 – 1 dhidi ya Leicester City kwenye mchezo wake wa kwanza wa ufunguzi wa kombe la ligi siku ya Ijumaa.
Tayari mshindi wa kombe la dunia mwaka 1998, Zidane akiwa na umri wa 46 amejiwekea rekodi nzuri baada ya kushinda mataji matatu mfululizo ya klabu bingwa barani Ulaya akiwa na Real, akichukua taji la La Liga, UEFA Super Cup mara mbili na FIFA Club World Cup mara mbili.