Michezo

Zinedine Zidane kurithi mikoba ya Mourinho Manchester United

Aliyekuwa meneja wa Real Madrid, Zinedine Zidane ameoneshania ya kuhitaji kuifundisha klabu ya Manchester United na kurithi mikoba ya Jose Mourinho msimu ujao wa ligi.

Zinedine Zidane 'is interested in managing Manchester United' according to L'Equipe

 

Kwa mujibu wa gazeti la L’Equipe  kutoka nchini Ufaransa Daily Mil,  METRO na  Mirror  vimesema kuwa Zidane anajipanga kutua ligi ya Uingereza hasa ndani ya klabu ya Manchester United.

The Frenchman stepped down as Real Madrid manager at the end of last season

Zidane ambaye ni raia wa Ufaransa aliiyacha klabu yake ya Madrid baada ya kuipatia jumla ya mataji matatu mfululizo ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Portuguese boss Jose Mourinho is entering his third season in charge of Manchester United 

Mfaransa huyo aliwahi pia kuhusishwa na kuhitaji kuinoa timu yake ya taifa lakini meneja Didier Deschamps aliamua kuendelea na majukumu yake mara baada ya kutwaa ubingwa wa dunia nchini Urusi.

Mourinho ameingia kwenye mgogoro na makamu mwenyekiti wa Old Trafford, Ed Wood kwenye kipindi cha maandalizi ya kuanza msimu mpya ligi kufuatia kulalamikia kukosa kusajili wachezaji wliyowahitaji.

Zidane 'has set his sights on a job in the Premier League and could replace Jose Mourinho'

Historia yake ya kutomaliza misimu mitatu ndani ya klabu moja imekuwa nichangamoto kubwa kwa Mreno huyo, hata hivyo amefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabo 2 – 1 dhidi ya Leicester City kwenye mchezo wake wa kwanza wa ufunguzi wa kombe la ligi siku ya Ijumaa.

Tayari mshindi wa kombe la dunia mwaka 1998, Zidane akiwa na umri wa 46 amejiwekea rekodi nzuri baada ya kushinda mataji matatu mfululizo ya klabu bingwa barani Ulaya akiwa na Real, akichukua taji la La Liga, UEFA Super Cup mara mbili na FIFA Club World Cup mara mbili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents