BASATA yakanusha kuufungulia wimbo wa ‘Mwanza’, latoa tamko kali kwa Rayvanny
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetoa tamko kwa umma, vyombo vya habari na jamii kwa ujumla kuwa halijaufungulia wimbo wa ‘Mwanza’, uliyoimbwa na msanii wa WCB, Rayvanny kwa kushirikiana na DiamondPlatnumz.
Baraza yatoa tamko kwa umma, vyombo vya habari na jamii kwa ujumla kuwa halijaufungulia wimbo wa 'mwanza'.
Baraza daima limekuwa likifanya kazi zake kwa weledi mkubwa na kuzingatia… https://t.co/O2vjYCnmMt
— Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) (@BasataTanzania) November 17, 2018
BASATA imesisitiza kuwa daima limekuwa likifanya kazi zake kwa weledi mkubwa na kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo iliyopo. Hivyo taarifa za kufunguliwa wimbo huo sio za kweli ni za kizushi, aidha jamii inatakiwa kuzipuuza taarifa hizo ambazo hazina chanzo maalum.