Kocha wa timu ya Young African, Nasreddine Nabi amefungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuwashambulia kwa maneno mwamuzi wa kati na mwamuzi wa akiba wa mchezo wao dhidi ya Ihefu FC uliyomalizika kwa kufungwa 2-1.
Nabi aliendelea kufanya kitendo hicho hata baada ya kuonywa kwa kadi ya manjano.
Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 42:2(2.1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.