Habari
Mbivu Mbichi Leo: Kitime Jaji Mkuu wa Tuzo TMA, aeleza jopo la watu 80 ilivyowapata washindi
Mwanamuziki wa muda mrefu na Jaji Mkuu wa Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) @john_kitime amefunguka juu ya mchakato wa kuwapata washindi wa Tuzo mbalimbali ambao watatangazwa usiku wa leo.
Kitime amedai zaidi ya watu 80 wamefanya uchambuzi yakinifu katika kuhakikisha washindi wanapatikana kihalali.
Mdau huo wa muziki amesema baada ya kusimamia tuzo hizo wameandika ripoti kwa @basata.tanzania kwaajili ya maoni yao.
Pia amewataka wasanii kuongeza ushiriki katika tuzo hizo pekee ya muziki nchini Tanzania.