Ubabaishaji: Tuzo za Madj wa Afrika ‘AGDAAwards 2013’ zaahirishwa
Baada ya kupigiwa promo kwa miezi kadhaa, tuzo za kwanza zilizoundwa kwaajili ya kuwatuza madj bora wa Afrika, African Global DJ Awards- AGDA Awards 2013 zimeahirishwa.
Tuzo hizo zilikuwa zifanyike Jumamosi, July 13 nchini Nigeria.Kupitia ukurasa wao wa Facebook waandaaji hao wameandika:
We want to announce the official cancellation of AGDAAwards 2013. More on this would be made know on this page and other social media platforms run by the organization. We are sorry for inconveniences caused by this cancellation and who sent out a release to explain reason why this had to be.
Rapper wa Uganda, Navio alikuwa amepangwa kuwa host wa tuzo hizo. Kufuatia tangazo hilo, waandaji wameshambuliwa kwa lundo la maneno ya kejeli kutokana na kuonekana ni wababaishaji.