Cassper Nyovest aweka historia kwa kuwa msanii wa kwanza wa Afrika Kusini kujaza ukumbi wa watu 20,000
Rapper wa Afrika Kusini, Cassper Nyovest ameweka historia kwa kuwa msanii wa kwanza wa nchi hiyo kujaza ukumbi wa The Dome ulioko jijini Johannesburg kwenye show aliyoandaa mwenyewe iliyofanyika Jumamosi Oct.31.
Cappser pia ndiye msanii wa kwanza wa Afrika Kusini kuutumia ukumbi huo wenye uwezo wa kujaza watu 20,000 ambao hutumika zaidi kwenye show zinazokuwa na wasanii wa kimataifa.
Show hiyo imemgharimu Cassper Rand milioni 4 (zaidi ya shilingi milioni 630) katika maandalizi.
Rapper huyo amejiwekea malengo ya kuweka rekodi nyingine mwakani, kwa kuahidi kufanya show nyingine kwenye uwanja mkubwa zaidi wa ‘Orlando stadium’ wenye uwezo wa kujaza watu 40,000 ambayo ni mara mbili ya The Dome.
Next year I'm doing Orlando stadium. 40 000 people . https://t.co/068SeTSR2M
— October 31st TheDome (@CassperNyovest) October 26, 2015