Chidi Benz amsihi Nikki Mbishi asiache muziki kama alivyotangaza
Kauli ya Nikki Mbishi kuwa ameamua kuacha muziki imewashtua wengi huku mashabiki wake wakimsihi kuwa aendelee kupambana.
Mmoja wa wasanii waliomsihi asichukue uamuzi huo ni Chidi Benz aliyedai kuwa yale ambayo Nikki anayapitia kwenye muziki ni ya kawaida na yeye amewahi kukukabiliana nayo.
“Nakanusha habari za Nikki mbishi kuacha mziki,nimeongea nae kama kaka na kumgusia mengi,najua amenielewa na nimemwambia asikubali wale wanaomkubali waanze kukubali wengine.mimi nimekumbana na vingi na watu weengi waliaminishwa kama nimeshushwa kimziki,jimefanyiwa mengi ambayo kwa muda ule nsingeweza kuelezea kila mtu nini kinaendelea,so if kikitokea kibaya kinatangazwa mpk kwenye taarifa za habari mbona mziki hauchezwi?ningekua sina nguvu hio nisingesumbua watu kuniweka front page..but bado nipo na nimekomaa.na naishi na naona wanaopewa kipaumbele na najua bado mimi ni mimi.Iron.”