Chris Brown kuachia mixtape mpya Ijumaa, siku ambayo Dreezy ‘Views’
Chris Brown anatarajia kuachia mixtape mpya aliyoipa jina “OHB Mixtape(Original Hood Bosses)itakayotoka Ijumaa hii. Drake pia anaachia album yake Ijumaa hii.
Ni baada ya kuachia ngoma mbili, Wrist (Remix) aliyowashirikisha Jeezy na Young Thug pamoja na Shut Down.
Hii ni teaser ya track mpya kutoka kwenye mixtape hiyo
https://youtu.be/wG1kpZnUB7M
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Breezy aliwataarifu mashabiki wake wanaoisubiri pia documentary yake, ‘Welcome To My Life’, alithibitisha kuachiwa kwa mixtape hiyo ambayo ni ya ushirikiano itakayowajumuisha wasanii tofaouti.
Pamoja na hivyo Chris Brown ametoa kionjo cha track itakayofuata kuachiwa kwenye mixtape hiyo inayoitwa ‘Whippin’ ambayo amewashirikisha Section Boys & Quayo ambayo pia itafuatiwa na ngoma ya pekee kutoka kwake itakayotoka May 5 mwaka huu.