Michezo
FA lazitupa t-shirt 4,000 zenye nukuu ya Sam Allardyce zilizokuwa zigawiwe baada ya mechi ya England na Malta
Chama cha soka nchini Uingereza, FA kimelazimika kuzitupa t-shirt 4,000 zilizokuwa zimepangwa kugawiwa kwa mashabiki baada ya mechi ya England na Malta sababu zilikuwa na nukuu ya kocha aliyetimuliwa, Sam Allardyce.
Allardyce, 61, alikuwa akijiandaa na mechi na mechi October 8 lakini kibarua chake kiliota mbawa baada ya kashfa yake ya rushwa kuibuliwa.
FA ilitaka kuzitumia t-shirt hizo kama kumbukumbu ya mchezo wake wa kusaka nafasi ya kushiriki kombe la dunia. Zilikuwa zimeandikwa ‘The journey starts with us all pulling together’ — kitu ambacho Allardyce alikisema siku ameteuliwa.