Burudani

Hanscana: Director anayenipa changamoto ni Godfather,mtu ambaye hatushei wateja huwezi kuwa challenge yangu

Director Hanscana ambaye ameonekana kuwa miongoni mwa watengenezaji wapya wa video wanaofanya vizuri kwa sasa Tanzania, amesema kuwa madirector wakubwa wa nje ndio wanaompa changamoto kwa sababu ndio anaowatazama zaidi.

Hans na Diamond
Hanscana, Diamond na Tudd Thomas

Akizungumza kupitia Planet Bongo ya EATV, Hanscana aliulizwa na mtangazaji wa kipindi hicho Dullah kuhusu ushindani uliopo kwenye upande wa utengenezaji wa video.

Swali: Ushindani uko vipi kwenye soko kwa kijana kama wewe mpya ambaye unakuja kwenye upande huu- Dullah

“Ushindani ni mkubwa sana kwenye soko, kuna malegend halafu kuna si malegend ila wanafanya vizuri kwa kiasi chao. By the way sio challenge kwangu kwasababu sio focus yangu,” alisema Hanscana.

“challenge inatokea katika kile ambacho unaki focus, ila wao si focus yangu kwahiyo sio challenge yani hawani challenge mimi kabisa. Ambaye mi wanani challenge ni Godfather kwasababu Godfather anashoot video na Diamond na Hanscana anashoot na Diamond, kwahiyo yule mi ni challenge yangu, ananichallenge labda Nicky Campos ambaye anashoot video na Vanessa Mdee na mi nashoot na Vanessa kwahiyo wale ndo wananichallenge kina Moe Musa ambao tunashare nao wateja, mtu ambaye hatushei wateja huwezi ukawa ni challenge yangu.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents