HabariUncategorized
Jeshi la Polisi Dar laeleza kuhusu kupishana kauli na Polisi Iringa juu ya tukio la kupotea kwa Abdul Nondo
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam leo Machi 16, 2018 limetolea maelezo juu ya tuhuma za kupishana kauli na jeshi la polisi Iringa kuhusu tukio la kupotea kwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Abdul Nondo aliyedaiwa kutekwa wiki mbili zilizopita.
Msikilize Kamanda Mambosasa akizungumzia kupishana kwa kauli hizo ambapo awali Polisi Iringa walisema Abdul alijipeleka mwenyewe kituoni na Polisi Dar wakasema alikamatwa.