Habari

Kampuni ya Singapore kuwekeza dola bilioni 1.3 kwenye visima vya gesi nchini

Kampuni ya Pavilion Energy Pte, ya nchini Singapore itawekeza dola bilioni 1.3 kwaajili ya kumiliki asilimia 20 ya umiliki wa visima vitatu vya gesi nchini Tanzania.

ieBqzD214w9o
Mwenyekiti Mtendaji wa Pavilion Energy Pte, Seah Moon Ming

Pavilion Energy, inayomilikiwa na Temasek Holdings Pte, iliingia kwenye makubaliano na kampuni ya Ophir Energy Plc (OPHR), ambayo inamiliki asilimia 40 ya cubic feet trilioni 15 za gesi kwenye visima vitatu, ilisema jana kwenye maelezo yake.

“Uendelezaji wa gesi asilia nchini Tanzania una faida kubwa, si tu kwa Pavilion Energy lakini pia kwa Singapore na Asia,” Hassan Marican ambaye ni mwenyekiti wa Pavilion, alisema kwenye maelezo yake.

Kampuni ya Berkshire, ya Uingereza inamiliki asilimia 60 ya visima hivyo.

Source: http://www.bloomberg.com

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents