Burudani

Kanye West abadili jina la album yake mpya anayotarajia kuitoa

Rapper Kanye West amefanya mabadiliko ya jina la album yake mpya anayotarajia kuitoa mwaka huu, ambayo mwanzoni aliita ‘So Help Me God’.

wpid-kanye-west-655x435.jpg

Album hiyo sasa itaitwa ‘SWISH’.

Kanye alitangaza mabadiliko hayo kupitia Twitter na kusema kuwa hata jina hilo la sasa linaweza pia kubadilika muda wowote.

“I’m changing my album name to ‘SWISH'” na baadae akaongeza tweet nyingine “I might change it again but that’s the name now.” .

Bado hajaweka wazi tarehe rasmi ya kutoka kwa album hiyo lakini itakuwa mwaka huu 2015.

‘SWISH’ itakuwa ni album ya sita kwa rapper huyo baada ya ‘Yeezuz’ iliyotoka mwaka 2013.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents