Michezo

Kitabu cha Sir Alex Ferguson ‘My Autobiography’ chavunja rekodi kwa kununuliwa kama ‘njugu’

Kitabu cha Sir Alex Ferguson, kimevunja rekodi kwa kuwa kitabu kisicho na mambo ya kutunga (non-fiction) kinachouzika kwa kasi zaidi.

article-2479870-190D953A00000578-701_634x406

Kitabu chake kilichokuwa kikisubiriwa kwa hamu kiitwacho ‘My Autobiography’, kimeuza kopi 115,547 katika wiki moja.

Kitabu cha Fergie ambacho kinauzwa kwa paundi £25 – kimeuza zaidi kwa wiki moja tangu miaka 15 iliyopita, kwa mujibu wa jarida The Bookseller. Rekodi ya awali ilishikiliwa na kitabu cha Delia Smith, How To Cook: Book Two kilichouza kopi 112,000 katika wiki ya kwanza, miaka 14 iliyopita.

article-2479870-18F393D400000578-535_634x362

Kitabu cha Sir Alex kimezidi vitabu vingine vya watu maarufu wa Uingereza kama kile cha Tony Blair, A Journey kilichouza kopi 92,000 miaka mitatu iliyopita na cha David Beckham, My Side, kilichouza kopi 86,000 katika wiki ya kwanza miaka 10 iliyopita.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents