Michezo
Klabu ya Simba ina nafasi ya kurejea kileleni leo ikiifunga Ndanda FC ya Mtwara
Klabu ya Simba SC leo itakuwa ina nafasi ya kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iwapo itashinda dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara.
Simba wanaikaribisha Ndanda leo katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakihitaji ushindi ili kuongoza ligi.
Na kocha wa Wekundu hao wa Msimbazi, Jackson Mayanja amesema kwamba timu yake ipo vizuri baada ya maandalizi ya tangu Jumatatu.
“Tunatarajia mchezo mgumu na wenye ushindani mkubwa, lakini tumejiandaa kushinda,”amesema Mayanja.