Burudani
Picha: Davido asherehekea dili la Sony, aeleza masharti aliyowapa hadi akakubali kusaini
Davido amesherehekea dili lake la Sony Music nchini Nigeria. Kwenye sherehe hiyo, watu maarufu kwenye kiwanda cha muziki nchini humo walihudhuria.
Alichukua pia fursa kuelezea mkataba wao. “Nilitumia karibu mwaka mzima kwenda na kurudi hadi dili hii kukamilika,” alisema. “Nilitaka kuhakikisha kuwa naendelea kubaki na udhibiti wa kazi yangu na kwamba vigezo vya dili hii vilikuwa vizuri kwangu.”
Aliongeza kuwa album yake itatoka baadaye mwaka huu na ataachia wimbo mpya mwezi huu. Tazama picha zaidi za event hiyo.