Michezo

Kocha wa Liverpool, Jürgen Klopp awaonya Real Madrid ‘hakuna aliyejua tungefika hapa’ (+video)

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ameitahadharisha klabu ya Real Madrid kuelekea mchezo wao wa fainali wa klabu bingwa barani Ulaya hapo kesho Mei 26, 2018.

Jurgen Klopp

Klopp amesema kuwa anafahamu fika klabu yake haina uwezo mkubwa kulinganisha na wapinzani wao Real Madrid lakini hiyo siyo sababu kwa Madrid kuwapeza kwani wana historia nzuri kwenye mechi kubwa.

Sisi ni Liverpool sio timu mzuri pekee hata hao (Real Madrid) lakini tuna vina saba vya  kufanya vizuri kwenye mechi kubwa. Hakuna aliyejua kama tutafika hapa lakini leo hii tupo hapa na hii ni kwa sababu sisi ni Liverpool.“amesema Jugen Klopp kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari jioni ya leo mjini Kiev, Ukraine.

Wengine waliotoa mitazamo yao ni wachezaji wa Liverpool, Van Dijk na Nahodha Jordan Brian Henderson ambao wote wamekiri kuwa gemu ni nzito ila wataushangaza ulimwengu.

Tazama press hiyo hapa chini na kuangalia wachezaji wa liverpool wakifanya mazoezi yao ya mwisho kuelekea kesho kwenye fainali vs Real Madrid.

https://youtu.be/tp3gelT_U4g

_______________________________________________________________________________________________

Kwa sasa unaweza kupata habari zetu zote sehemu moja kwa kupitia App yetu ya Bongo5. Pakua sasa kupitia Play Store kwa kubonyeza link hii – https://bit.ly/2J2Argw

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents