Burudani

Linah: Nimeshatambulishwa kwa wakwe zangu Uganda

Linah anadai tayari ameshatambulishwa kwa wazazi wa mpenzi wake mpya ambaye ni raia wa Uganda, Williams Bugeme.

11375190_749899448489507_1468429550_n

Hata hivyo Linah ameiambia Bongo5 kuwa sasa hivi wameamua kupunguza kujionyesha sana ili wapate muda wa kufanya kazi.

“Namshukuru Mungu mama mkwe alinipokea vizuri sana,” Linah ametuambia. “Wadogo zake pamoja na marafiki. Najivunia kuwa naye sema sasa hivi tumeamua tupunguze kujionyesha. Kama mapenzi yapo tu huu ni wakati wa kufanya kazi kwanza,” ameongeza.

Kwa upande mwingine Linah ambaye ni miongoni mwa wasanii waliotajwa kuwania tuzo za kimataifa za Afrima, amewataka watanzania kuunga mkono kazi zake pamoja na kumpigia kura.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents